user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Nawasalimu Makada wote wa Chama Cha Kimonunisti Kenya na Wageni wote waalikwa. Siku ya leo ambayo ni siku muhimu sana yakuadhimisha na kuwasherehekea wafanyikazi wote duniani. 

Leo tunajumuika hapa Kisumu lakini sisi ni baadhi tu ya wavujajasho wengi waliojumuika katika kila Pembe ya dunia kusherehekea nguvu Kazi ya wavujajasho duniani.

Lakini, Kuna nini  chakusheherekea kwa  wafanyikazi ? Wakati mabilioni ya wafanyikazi wanaendelea kukandamizwa na mfumo wa kiimla wa ubepari. Mfanyikazi hana chochote chakusheherekea katika jamii yenye inaongozwa na  uimla wa mtaji wakibinafsi dhidhi ya maslahi ya wanaotengeneza mtaji huo.

Jamii yetu imegawanyika baina ya wavunajasho wachache wanao miliki nyenzo za uzalishaji na wanaozitumia kunyonya nguvukazi ya wavujajasho wengi ambao wanaendelea kuishi maisha ya kichochole.

Wafanyikazi wa Kenya kama wafanyikazi wengine wameenedelea kukandamizwa kwa kulipwa Mishahara duni na isiyoweza kukimu mahitaji yao, wafanyikazi wameendelea kufanya kazi masaa zaidi ya yale yanayotakikana na sheria za kufanya kazi duniani. Mazingira yakufanya Kazi yamezorota na wafanyikazi wengi wanapata ajali na hata magonjwa kutokana na Mazingira duni yakufanya kazi. 

Serikali ya Kenya haijaweka mikakati yoyote yakulinda maslahi ya wafanyikazi na hata kuongeza nguvukazi ya taifa lenye lina watu waliohitimu katika tajriba tofauti na ambao bado hawajapata kazi kwa sababu yakutoendeleza viwanda na kilimo ambayo ndiyo nguzo msingi ya nchi yeyote inayotaka kujiendeleza.

Mashirika yakimataifa kama Benki ya Dunia na IMF( International Monetary Fund) yameendelea kushinikiza matakwa ya ulibarali mamboleo ambayo yamekua na madhara makubwa kwa wafanyikazi na maisha ya mvujajasho wa Kenya.

Serikali hii ya kiimla pia imeendelea kusimamisha na kupinga juhudi zozote za wafanyikazi kuungana na kujitetea. Polisi wametumika kuwapiga wafanyikazi wakati wanapo fanya migomo na serikali imekataa kufuata mikataba ya makubaliano na wafanyikazi wa umma.

Vyama vya wafanyakazi na viongozi wa vyama hivi pia wamenunuliwa ili kulegeza kamba katika mapambano ya wafanyikazi. Sisi wakomunisti tukona na jukumu lakuenda miongoni  mwa wafanyikazi hawa na kuwapa mwamko Mpya wa kimawazo ili wabadilishe mambo yalivyo.

Sisi wakomunisti tunafaa kuendelea na kazi yakujenga vyama hivi vya wafanyikazi na kuleta mawazo ya kimapinduzi kwa wafanyikazi ili waelewe   uwezo walio nao. 

 Ingawaje,  vyama hivi vingine vimeshikiliwa na mabepari mchwara wanaotumia uongozi wao ili kuendelea kujinufaisha kibinafsi kama katibu mkuu wa COTU(Confederation of Trade Union) Bwana Francis Atwoli. Viongozi hawa ni kupe wanaonyonya jasho la wafanyikazi wakenya na lazima tuwapinge ki itikadi na tuwang'oe ili turejeshe hadhi ya vyama vya wafanyikazi wakati wa wazalendo kama Makhan Singh, Fred Kubai, Bildad Kaggia na Chege Kibacia.

Wakomunisti pia tunajukumu la kujenga Chama cha Kisiasa cha wafanyikazi CPM-K kwani tunapigana kuchukua uongozi na kujenga uimla wa wafanyikazi dhidhi ya wanaomilki mtaji, hii ndio njia yakujenga mfumo wa usoshialisti ili kuelekea katika mfumo wa kikomunisti ambapo hakuna ukandamizaji baina ya binadamu na binadamu mwingine.

Chama Chetu CPM-K ndicho kitapeleka harakati na gurudumu la wafanyikazi mbele ya mambo mengine ambayo vyama vingine vya wafanyikazi haviwezi kutekeleza. 

Makada wote wa Chama wanajukumu la kihistoria na la kijamii kujenga Chama mahali wanapofanyia kazi ili kuleta mawazo yakimapinduzi kwa wafanyikazi wengine, Chama chetu nicha wafanyikazi na lazima tukijenge miongoni mwa wafanyikazi wenyewe.

Chama chetu kitajaribu kuleta pia Wakulima na wavujajasho wengine katika jamii ili kuikomboa Kenya na dunia kutokana na maovu ya ubepari na ubeberu. Mapigano ya kwanza yakatukua dhidhi ya mabepari wa nyumbani wanaoendeleza maslahi ya mabeberu na mabepari wa nje kwa kufanya kazi ya kibaraka na kutumia vyombo vya dola venye vinamilikiwa na mabepari wa nje ili kukandamiza jamii.

Nawatakia mazungumzo yenye fanaka katika mkutano wa leo wakuadhimisha siku hii na tuendele kujenga Chama cha wafanyikazi.

 

Yadumu Mapambano ya wafanyikazi !!!

Idumu harakati za kujenga Usoshalisti!!!

Kidumu Chama Cha Wafanyikazi CPM-K !!!

Mwaivu Kaluka.

Mwenyekiti Wa Chama Cha Kikomunisti Umaksi - Kenya.

THE ESCALATING CRISIS OF FEMICIDE IN KENYA
02 Jun 2026 08:50

  STATEMENT BY THE STEERING COMMITTEE OF THE REVOLUTIONARY WOMEN’S LEAGUE   June 1, 2026    The Revolutionary Women’s League extends its deepest condolences to the families, friends and communities of all women whose lives have been stolen through femicide. We mourn every daughter, every mother, every sister, every wife, every domestic worker, every student, every worker, every queer woman and every woman whose life has been violently cut short.   We stand in solidarity with all those who continue to carry the pain of these losses. We do so not only as women, but as members of  [ ... ]

Read more
REFLECTIONS OF GENERAL SECRETARY BOOKER OMOLE ON HIS RECENT VISIT TO KATHMANDU, ...
02 Jun 2026 08:49

Expose and Defeat US Imperialism, the Primary Aggressor Against Humanity May 26th, 2026   Nepal is a land of immense revolutionary history and immense contradiction. The mountains of Nepal carry the memory of armed struggle, sacrifice, and the blood of workers and peasants who rose against feudal monarchy and imperialist domination. Through the communist led anti monarchy insurgency, the old order was shaken violently. The 2001 royal massacre accelerated the collapse of feudal authority and opened the road toward the struggle for national democracy. During the ten years of People’s War,  [ ... ]

Read more
BONIFACE MWANGI, GUANTANAMO BAY, AND THE HYPOCRISY OF US SANCTIONS: STATEMENT TO...
23 May 2026 11:52

  The Communist Party Marxist Kenya notes the recent sanctions imposed by the United States government against a Tanzanian police official over the torture involving Kenyan activist Boniface Mwangi and Ugandan activist Agather Atuhaire.   As revolutionaries and defenders of democratic rights, we firmly condemn torture, arbitrary detention, repression, disappearances, and attacks against activists, workers, peasants, journalists, opposition forces, and progressive voices anywhere in Africa. The suffering of the people can never be normalised. State violence against the masses remains react [ ... ]

Read more
Fascism in the African Neocolonies Imperialist Crisis, and the Struggle for Nat...
22 May 2026 05:30

  Booker Omole, General Secretary, Communist Party Marxist Kenya
repared for the International Theoretical Conference on Fascism and Imperialism in the 21st Century in the Neocolonies
Kathmandu, Nepal
22 to 23 May 2026 Imperialism in Crisis and the Return of Fascism   The Communist Party Marxist Kenya extends militant proletarian greetings to all revolutionary organisations, communist parties, anti-imperialist formations, workers movements, youth organisations, and progressive intellectuals gathered at this important international theoretical conference in Kathmandu, Nepal.   This confe [ ... ]

Read more