user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Enyi wafanyikazi

Wafanyikazi wavujajasho

Mnaomenyeka katika viwanda vya mabeberu

Mnaokamuliwa jasho na mabepari

Huko Nairobi na Mombasa na Kisumu na Eldoret na Thika

Na Nakuru na Nanyuki na Adhi River na Kitengela na Naivasha na Machakos

Mnaotumika katika mashamba viwanda vya miwa

Mumias na Miwani na Muhoroni na Nzoia na Soni

Mnaovuja jasho katika mashamba ya chai

Kericho na Limuru na Kisii na Nyeri na Murang'a

Katika mashamba ya kahawa

Kiambu na Murang'a na Kisii na Embu na Meru na Kirinyaga

Wafanyikazi katika mashamba ya mahindi na ngano

Transnzoia na Uasingishu na Nakuru na Bungoma na Narok

Mnaofanya kazi usiku na mchana katika mashamba ya mikonge

Mwatate na Taveta na Voi na Kibwezi na Kilifi

Katika mashamba ya Korosho Pwani

Katika mashamba ya mananasi Thika

Katika mashamba ya maua Naivasha na Adhi River

Katika mashamba ya mifugo Taita na Laikipia na Nakuru

Wafanyikazi katika mahoteli ya watalii

Nairobi na Mombasa na Malindi na Nyeri na Bura na Tsavo

Na Amboseli na Lodwar na Kisumu na Nakuru na Naivasha

Wafanyikazi wa migodi

Magadi na Adhi River na Bamburi na Taita na Iteni

Wafanyikazi wa bandarini na maofisini na vyuo vya elimu

Wafanyikazi wa ujenzi wa nyumba na barabara

Wafanyikazi wote wa Kenya

Wafanyikazi wa Afrika Mashariki

Wafanyikazi wa Afrika

Wafanyikazi wa ulimwenguni

Popote pale mlipo duniani

Endeleeni kuuitikia mwito wa Karl Marx:

Enyi wafanyikazi

Wavujajasho wa ulimwenguni kote

Kutokana na juhudi zenu

Kutokana na kutiririka kwa jasho lenu

Kutokana na kumenyeka kwa viungo vyenu

Tunakula

Tunavaa

Tunalala

Tunasafiri

Tunaburudika na kustarehe

Mikono yenu inachora dunia yetu

Kwa bandari na barabara na reli na barste tilatila

Misuli yenu inatupambia sayari yetu

Kwa nyumba na majumba na magorofa mzomzo

Jasho linalomtiririka

Linatupa magari na meli na ndege na vyombo sufufu

Na makompyuta na mitambo na mashini za kila aina

Hakika kazi yenu wafanyikazi

Ndiyo inayotafsiri sayansi na tekinolojia

Katika lugha halisi ya uzalishaji

Kwani nyinyi, enyi wavujajasho popote pale mlipo

Nyinyi ndiyo shina la utamaduni halisi

Ndiyo damu na mifupa ya uhai wa jamii

Ndiyo pumzi na nyenzo za maendeleo ya binadamu

Pasipo nyinyi, enyi wafanyikazi popote pale mnapoishi

Pasipo kazi yenu, jitihada zenu

Kila kitu kitasimama, hata maisha ya ustaarabu

Kwa vile nyie mnaoitwa wafanyikazi, wavujajasho

Nyinyi ndiyo msingi hasa

Wa ungwana na ustaarabu uliyoko duniani

Ndiyo nguvu zinazosababisha mageuzi

Wafanyikazi mu wasanii wa kubadilisha sura ya maumbile

Kwa bidii yenu

Matunda ya ufanisi wa sayansi na tekinolojia yanaliwa

Ndiyo, kazi- nguvukazi

Ndiyo iliyomuumba mtu

Kazi ndiyo iliyomleta binadamu akawa binadamu

Ndiyo iliyomkokota kutoka kwa maumbile

Ikamtenganisha na mnyama

Na kumtia katika mkondo wa historia

Kwa kazi yenu, enyi wafanyikazi tangu kale na sasa

Tunazidisha pengo kati yetu na wanyama

Kwa hivyo, wafanyikazi

Enyi wavujajasho, wazalishaji mali

Tambueni umuhimu wenu!

Tambueni umuhimu wenu wafanyikazi popote pale mlipo!

Bila nyinyi hakuna historia

Pasina uzalishaji na wazalishaji maisha yatasimama

Lakini

Enyi wafanyikazi

Enyi wafakazi mnaokufa kwa kazi

Wafanyikazi wa nchi yangu

Wafanyikazi wa Afrika Mashariki

Wafanyikazi wa Afrika bara langu

Wafanyikazi wa ulimwenguni kote

Ulimwengu uliyotekwa nyara na mfumo wa kinyama wa ubeberu

Katika mataifa yaliyoko chini ya ukoloni-mamboleo

Penye jamii ya mfumo wa mwenyenguvu mpishe mnyonge msonge

Wafanyikazi mnaishi maisha magumu mno, maisha ya kinyama

Mmegeuzwa watumwa katika nchi zenu wenyewe

Maisha yenu enyi mfanyaokazi

Enyi mmenyekao

Enyi wafanyikazi wa Kenya taifa langu

Enyi wazalishaji chini ya ubepari na ubeberu

Ni maisha ya tabu dhiki na kusaga meno

Maisha ya umaskini ufukara na ukosefu

Maisha ya njaa na kiu cha kila mazuri

Maisha machungu ya upweke na ukiwa

Maisha ya ushenzi ushirikina ulevi na ujinga

Maisha ya kugandamizwa na kunyanyaswa mbele na nyuma

Maisha ya hofu wasiwasi kiherehere na dukuduku

Maisha ya kutumiwa kutukanwa kudhalilishwa na kuonewa

Maisha ya kunyonywa na kutajirisha waajiri wenu

Maisha ya kuzalishia wachache katika jamii

Maisha chini ya imla na kuvunjwa kwa haki za binadamu

Maisha ya mashindano na mapambano kila kuchako

Enyi wafanyikazi wa Kenya, nchi yangu mzazi

Enyi wafanyikazi wa Afrika, bara linalochemka kwa ghamu na ghadhabu

Enyi wafanyikazi chini ya himaya ya ubeberu na ubepari

Mnaishi kwa shida, shida tupu

Shida ya inflesheni na ujira wa kitumwa

Shida ya kupunjwa na kulanguliwa juu na chini

Shida ya kutafuta karo za shule

Shida ya maradhi na kukosa dawa na matibabu

Shida ya ajali barabarani na viwandani

Shida ya ukosefu wa nyumba na kunyonywa na wenye nyumba

Shida ya uhalifu na wahalifu na maisha ya kimathare mijini

Shida ya machugachuga na mahangaiko ya ukosefu wa kazi

Shida ya kukamatwa kuteswa kufungwa na kuuawa na wahalifu na polisi

Shida ya ukabila upendeleo na ubaguzi wa rangi

Shida ya ubaguzi wa kijinsia na kunyanyaswa kwa wanawake

Shida ya kutawalwa na wakora wasaliti walafi wajinga

Shida ya hofu ya nyakati za uzeeni

Maisha ya shida ghasia mizozo na gandamizo

Hamna raha ndugu wafanyikazi hamna katu hamnani

Matunda ya jasho lenu yanaliwa na mabepari na jamaa zao

Utamaduni halisi mnaouzalisha ni kwa ajili ya tabaka la wanyonyaji

Oh wafanyikazi wa nchi yangu

Mnaonyonywa katika viwanda vya mabeberu nchini

Mnaotumishwa katika mahoteli ya mabepari wa kimataifa

Mnaochapishwa kazi kwa mashamba ya wakoloni-mamboleo

Mnaohangaishwa katika makampuni na biashara za wageni

Umaskini wenu ni utajiri wa Ulaya, Marekani na Japan

Jasho lenu linafaidi mataifa yanayotunyonya

Juhudi zenu hazitumiki kuboresha maisha katika taifa lenu

Mazao ya akili na misuli yenu yanang'wafuliwa na wanyonyaji wa nje

Dola la Kenya linashikilia na kulinda mirija ya kuwakamua

Serikali ya mahomugadi wa jana na leo inawasaliti kwa maadui zenu

Nalo tabaka la matajiri wa kienyeji ni waitifaki wa ubeberu

Mnauzwa na ndugu zenu wenyewe kwa pesa nane

Oh wafanyikazi wa nchi yangu ya kuzaliwa

Wafanyikazi wa Afrika Mashariki na Afrika

Ubeberu unamnyonya kama wafanyikazi na watu weusi

Unatumia ukabila na ubaguzi wa rangi kuzidisha kunyonywa kwenu

Enyi wanawake wafanyikazi wa nchi yetu

Mnanyonywa kama wafanyikazi kama watu weusi na kama wanawake

Mnaelewa hali yenu wafanyikazi mnajua ukatili mtendewao

Nyanyaso mnazonyanyaswa mnazielewa zaidi

Maonevu mnayoonewa mnayafahamu sana

Vilio mnavyolia mnaweza kuvieleza kwa marefu na mapana

Wambea wenu mnaishi nao mnajua ukatili wao juu chini

Itikadi na mbinu za kuwarubini lazima mzibaini bayana

Kwani daima mko katika harakati za kitabaka

Maadamu mazao yenu yanazidisha utumwa na mateso yenu

Na chini ya ukoloni-mamboleo

Chini ya dola la vibaraka wa mabeberu

Chini ya udikteta na ufashisti wa wasaliti

Hamna hata haki ya kuuza jasho lenu, sembuse uhuru!

Mwanyonywa vururumtende kwa msaada wa dola la wauzaji wa nchi

Polisi wanatumiwa kuvunja migomo na maandamano yenu

Sheria zimetungwa kuhalalisha kunyonywa na kunyanyaswa kwenu

Jela zinatumiwa kuwafunga mashujaa na waitifaki wenu

Propaganda zinasambazwa za kuwadanganya na kuwagawanya

Mnaleweshwa elimu ya ubepari na ushirikina kuparaganya mapambano yenu

Vyama bandia vya wafanyikazi vilivyoundwa na serikali

Vinamsaliti vinamuuza hadharani usiku na mchana

Enyi wafanyikazi wa Kenya

Msiosita kupambana

Hamna chama chenu cha wavujajasho hamna mnasema kila siku

Udikteta, utawala wa mbwa wa wanyonyaji wa nchi yetu

Unawapora haki yenu ya kuunda vyama huru vya wafanyikazi

Enyi wafanyikazi!

Wafanyikazi wa Kenya!

Wafanyikazi wa Afrika!

Wafanyikazi wa ulimwenguni!

Mna uwezo mkuu wa kujikomboa

Nguvu zenu zatosha kuvunja silisili zinazomfunga

Nyie ndie mnaoshikilia bomubomu

Za kuulipua mfumo wa kinyama wa kibepari

Ndiyo silaha kuu

Za kutukomboa kutoka kwa nyanyaso za ubeberu

Enyi wafanyikazi wa Kenya

Mliyoongoza mapambano ya uhuru

Mliyoshikilia tochi ya ukombozi katika vita vya Mau Mau

Hata leo jukumu ni lenu wafanyikazi

Hamna budi kuendelea kuwa katika mstari wa mbele

Katika vita dhidi ya udikteta na ukolonimamboleo

Wafanyikazi wa Afrika na dunia inayonyonywa na ubeberu

Wavujajasho na ndugu zenu wakulima-makabwela

Mnaonyonywa kuliko wafanyikazi katika nchi za kibepari

Mnaonyanyaswa kama wafanyikazi na kama taifa

Hakika ukombozi wenu ndiyo utakaokuwa msingi

Wa ukombozi wa wafanyikazi wa Ulaya na Marekani na Japan

Ukombozi kamili wa wote wanaonyanyaswa duniani

Enyi wafanyikazi

Nyinyi ndio mizizi ya kuhakikishia dunia

Kuchipuka na kukua kwa huru haki amani na furaha kamili

Wafanyikazi wa Kenya

Nyie ndio shina

Ya harakati za kidemokrasi

Pambaneni! Pambaneni! Pambaneni!

Popote mlipo nchini

Pambaneni! Pambaneni! Pambaneni!

Msirudi nyuma wala msikate tamaa hata siku moja

Pambaneni! Pambaneni! Pambaneni!

Usiku na mchana pambaneni!

Kupambana ni haki yenu pambaneni wafanyikazi wa Kenya!

Pambaneni dhidi ya waajiri na matajiri!

Pambanieni ujira bora na bora zaidi!

Pambanieni hali bora ya kuuza nguvukazi yenu!

Pambanieni haki ya kuwa na vyama huru vya wafanyikazi!

Pambanieni haki ya kuchagua viongozi wenu wenyewe!

Pambanieni haki ya kukutana kugoma na kuandamana!

Pambaneni dhidi ya wasaliti wanaomuuza kwa wanyonyaji!

Pambaneni dhidi ya vyama bandia mnavyoundiwa na dola!

Pambaneni dhidi ya mfumo wa imla!

Pambaneni dhidi ya kasumba ya kikoloni!

Pambaneni dhidi ya itikadi za kibwanyenye!

Pambaneni dhidi ya utamaduni wa hofu na kimya!

Pambaneni dhidi ya ukabila na ubaguzi wa rangi!

Pambaneni dhidi ya unyanyaswaji wa wanawake!

Pambaneni kwa matumaini ya ushindi wa ukombozi kamili

Hakika usoshalisti ndiyo mwokozi wenu

Ukomunisti ndiyo ukombozi kamili wa dunia upambanieni!

Itikadi ya Umarx-Ulenin daima iwe tochi na ngao yenu

Mapinduzi tu

Mapinduzi ya kisoshalisti

Ndiyo yatakayotuhakikishia uhuru wengi tunaonyonywa

Demokrasi ya kibepari isiwe mwisho wa mapambano yenu

Demokrasi iwe ngazi ya kuuvunjilia mbali mfumo wa kinyama wa ubepari

Demokrasi ya tabaka la wengi wanaonyanyaswa, dola linalodhibitiwa na wafanyikazi

Dola la kung’oa mizizi yote ya mfumo wa ubepari na ukoloni-mamboleo

Dola la kujenga na kulinda mfumo wa usoshalisti

Ndiyo shabaha ya harakati za kidemokrasi ya wafanyikazi

Pambaneni! pambaneni! pambaneni!

Pambaneni huku mkikumbuka umuhimu wenu kama wafanyikazi!

Pambaneni bila kusahau ndugu zenu wa kitabaka wakulima-makabwela!

Umoja wenu

Mshikamano madhubuti wa wavujajasho

Muungano wa wanaonyonywa na kugandamizwa

Usiojua kabila wala rangi

Unaokataa kubaguliwa kwa wanawake

Wenye kushikanishwa na gundi ya itikadi ya ukomunisti

Ndiyo silaha na hakika yenu ya ushindi!

Enyi wafanyikazi wachimbaji wa kaburi la ubepari

Mtakaozika mfumo wa udhalimu wa mtu kwa mtu

Unganeni! Unganeni! Unganeni kwa mapambano!

Popote mlipo unganeni wanaonyanyaswa wote!

Unganeni mpambane pasina kurudi nyuma

Hamna chochote cha kupoteza

Isipokuwa dhiki na nyanyaso za ubepari na ukoloni-mamboleo!

Hakika mapinduzi yenu wafanyikazi

Yatakuwa msingi wa kujenga mbingu hapa hapa duniani!

Yadumu mapambano ya wafanyikazi!

Zidumu harakati za uhuru wa wananchi wengi wa Kenya!

Udumu ukomunisti!

Adumu Makhan Singh, mkomunisti wa kwanza Kenya

Wadumu kina Chege Kibacia na Pio Gama Pinto na Isaak Gathanju

Na kina Harry Thuku na Bildad Kaggia na Mary Muthoni Nyanjiru wadumu

Wadumu mashujaa wa wafanyikazi wa Kenya

Yadumu majina ya kina Marx, Engels, Lenin na Stalin!

Wadumu kina Mao Tse Tung na Kim Il Sung na Fidel Castro na Che Guevara

Na Chris Hani na Julius Nyerere na Samora Machel na Amilcar Cabral na Agostino Neto

Na Kim Jong Il na Walter Rodney na Maurice Bishop wadumu na Joe Slovo

Zidumu fikra za kina Kwameh Nkuruma na Abdulrahman Mohamed Babu na Mamdani

Na fasihi za kina Shiraz Duran na Ngugi wa Thiong’o na Sembene Ousman

Na Shafi Adamu Shafi na Alex Laguma na Shaaban Robert na Chinua Achebe zidumu

Na zile za kina Felix Iyayi na Ahmed Said Mohamed na Ayi Kwei Armah zidumu pia

Zidumu fikra za kimapinduzi na mapinduzi Afrika

Na muungano wa kimapinduzi wa Afrika udumu

Wadumu wakomunisti popote walipo nchini na ulimwenguni!

Udumu umoja wa wafanyikazi wa kupambania ukombozi wa jamii!

Na iwe ni aluta Kontinuaaahhh hadi ukombozi kamili

Kenya

Na duniani!

 

Social Democratic Party of Kenya (SDP)

 

Mei 1 2015

  The Rural Woman: Not to Be Celebrated—But Liberated
24 Nov 2025 06:00

                                                                  peech on the Peasant Women Day, 15th October, 2025. Written by Leon Munala Secretary of The Peasants and Peasant Organization Delivered by Comrade Karimi Wa Kagendo National Organising Secretary, Revolutionary Youth League Comrades, sisters, and fellow workers! Today, the representatives of global capital in their glass palace tells us to celebrate. The United Nations, that grand committee for managing the common affairs of the global bourgeoisie, has  [ ... ]

Read more
FROM THE COMMUNE TO THE PEOPLE’S POWER: ANTI-IMPERIALIST STRUGGLE AND THE PATH O...
12 Nov 2025 08:41

    Booker Omole General Secretary, Communist Party Marxist Kenya (CPMK) October 17th, 2025 Caracas, Venezuela   omuna o Nada: The Question of Power in the Age of Imperialist War Comrades, the slogan “Comuna o Nada” — the commune or nothing — is not merely a Venezuelan proclamation; it is a universal cry of the proletariat in our epoch of crisis. It affirms that without transforming the relations of production, without uprooting imperialist domination, and without transferring power from the exploiting classes to the working people, there can be no socialism.   Today, [ ... ]

Read more
OFFICIAL STATEMENT ON THE FASCIST OFFENSIVE OF IMPERIALISM IN TANZANIA UNDER PR...
05 Nov 2025 14:01

November 2, 2025   The Communist Party Marxist Kenya stands with the people of Tanzania in this moment of heightened danger. The ruling class across East Africa is tightening the chains of monopoly finance capital. The mask of liberal democracy is falling. Behind it stands naked reaction. Behind it stands fascism in African colours.   President Samia Suluhu Hassan has presided over political developments marked by aggressive interference from foreign capital. We are witnessing new assaults by the corporations and financial institutions headquartered in the old imperial centres. They want [ ... ]

Read more
STATEMENT ON THE PASSING OF COMRADE KIM YONG NAM COMMUNIST PARTY MARXIST KENY...
05 Nov 2025 13:51

    November 5, 2025   The Communist Party Marxist Kenya conveys its deepest condolences to the Workers Party of Korea, the Government of the Democratic People’s Republic of Korea, and the heroic Korean people on the passing of Comrade Kim Yong Nam, former Chairman of the Standing Committee of the Supreme People’s Assembly.   Comrade Kim Yong Nam was not merely a statesman. He was a defender of sovereignty. He was a guardian of independence. He was a steadfast revolutionary in the global front against imperialism.   Throughout his service to the Party and the State, the Dem [ ... ]

Read more