user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

“Utekelezaji wa sera za kibepari nchini umetuumiza sisi wananchi tuliyo wengi. Ubinafsishaji wa ardhi, migodi, mbuga za wanyamapori na maliasili zingine umetupora sisi tuliyo wengi haki za umilikaji na matumizi ya ardhi zetu za jadi tulizozirithi kutoka kwa mabibi na mababu zetu. Badala yake serikali inashirikiana na wawekezaji (mabepari) wa nchini na wa kigeni kutunyonya, kutunyanyasa, kutuvunjia heshima, kuvuraga utamaduni wetu na haki zetu za binadamu kiholela. Mfumo wa ubepari na ubinafsishaji unaoendelea hauwezi kutukomboa kutoka kwa ufukara na kutuletea maendeleo endelevu kwani unapanua pengo kati ya matajiri na masikini. Lazima tujizatiti na kuungana kupambania kurudi kwa Azimio la Arusha!”.

Hayo na mengine yalisemwa na kuazimiwa na jamii za wakulima, wachungaji, mashirika ya umma na Watanzania makabwela ambao walishiriki katika Kongamano la Saba la tamasha ya wasomi ya kumuenzi baba wa taifa la Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kongamano hilo lililofanyika kutoka tarehe 13 hadi 15 Aprili mwaka huu katika Ukumbi wa Nkuruma katika Chuo Kikuu cha Dar - es - saalamu liliandaliwa na Kigoda cha Nyerere chuoni hicho chini ya uwenyekiti wa Profesa Peminah Mlama. Pamoja na watu kutoka mashinani, Kongamano hilo lilishirikisha wasomi na wanafunzi wa chuo kikuu na wa shule za upili ambao walilalamika jinsi wawoto wa makabwela wanavyozidi kunyimwa fursa ya kupata elimu bora kutokana na ubinafsishwaji wa taasisi za elimu nchini Tanzania. Wanafunzi wa chuo kikuu walilalamika kuhusu ukame wa demokrasi ya kitaaluma katika vyuo vikuu iliyoandamana na ubinafsishwaji wa elimu katika nchi hiyo. Kongamano hilo lilisisimuliwa na wanafunzi wa shule za upili waliyolalamika kwa ufasaha kuwa elimu sasa inawafundisha watoto maadili ya ubinafsi, ulafi na kutojali binadamu wengine badala ya yale ya kiutu na kizalendo yaliyokuwa yakifundishwa na mwasisi wa taifa lao, Nyerere.

Wawakilishi wa jumuia za wakulima na wachungaji kutoka Loliondo, Kilosa, Mbeya, Geita walieleza kwa uchungu kuhusu masaibu wanayolazimika kuishi nayo kutokana na kunyanyaswa na kuporwa haki juu ya ardhi na maliasili zao na wawekezaji wa Kitanzania na kigeni ambao sasa wanapendelewa na serikali dhidi ya jumuia. Kongamano lilisikitishwa na maelezo kuhusu uvunjwaji wa haki za binadamu za wakulima na wachungaji wanaoishi katika maeneo ya migodi ya Geita, Shinyanga na Mwanza. Kilio hichihicho kililiwa na wakulima makabwela wa mpunga kutoka Mbeya waliyonyang’anywa ardhi zao na wajasiriamali na serikali. Pia jumuia za wakulima na wachungaji za Kilosa katika Mkoa wa Morogoro zilisimulia jinsi dhuluma na migogoro ilivyozidi sehemu zao kutokana na uvamizi na unyakuzi wa ardhi unaoendelea kutokana na ubinafsishaji.

Aidha, wanaharakati wa kupigania haki za kijamii kutoka Kampala na Moroto Uganda walishiriki na vilevile mashirika ya umma ya Kenya mkiwemo shirika la haki za kijinsia, shirika la kupigania haki ya maji na shirika la kupigania haki ya ardhi ya umma huko Garissa. Nikiwa mwenyekiti wa chama cha Social Democratic Party of Kenya (SDP) niliongoza ujumbe wa wanachama wanne kushiriki kongamano hilo maarufu.

Mada kuu ya kongamano hilo ilikuwa ubinafsishaji na haki za kijamii. Shabaha ya mada hii ilikuwa ni kutathmini athari za kiuchumi, kisiasa, kijamii na kitamaduni za marekebisho ya kiuchumi yaliyotoa Tanzania kutoka barabara ya Azimio la Arusha (ujamaa) na kuitia katika barabara ya ubeparimamboleo. Baada ya Nyerere kung’atuka kutoka kwa urais wa Jamhuri ya Tanzania na pia uwenyekiti wa chama tawala, Chama cha Mapinduzi (CCM), rais Ali Hassan Mwinyi aliyechukua nafasi yake alianza marekebisho ya kiuchumi ya kibepari katika nchi hiyo. Rais Benjamini Mkapa alimrithi Mwinyi na kuendelea kuzingatia sera za Rais Mwinyi za ruksa ya kuuvunja mfumo wa ujamaa na kujitegemea na kuelekeza Tanzania katika mfumo wa ubepari. Hivi leo Tanzania ikiongozwa na Rais wa nne Jakayo Mrisho Kiketwe inaendelea kutekeleza sera za ubepari na ukolonimamboleo kwa fujo.

Huku ikiwa katika mfumo wa ubepari, uchumi wa Tanzania umekua kwa kasi sana (kwa zaidi ya asilimia saba). Barabara nyingi za lami zimejengwa mijini na mikoani. Katika kila miji ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Dar - es - saalamu, Dodoma, Tanga, Mbeya, Arusha, Mwanza na Moshi majumba makubwa ya ghorofa yanaota kila kuchako. Aidha, mitaa ya kifahari wanakokaa matajiri yenye majumba makubwa na ya kupendeza ajabu nayo pia ni dhihirisho la kunoga kwa uchumi wa ubepari. Vilevile, masupamaketi ya kukidhia haja za tabaka la mabwanyenye na magari ya kifahari yamejaa kila sehemu mijini. Ardhi, migodi na mashirika ya umma yamezidi kubinafsishwa na kuuziwa (kupewa) mabepari wa Tanzania na nchi za kigeni. Wawekezaji kutoka kila pahali ulimwenguni wanakimbilia Tanzania kuwekeza na kununua mali ya umma ya viwanda, biashara, ardhi, madini, wanyamapori na maliasili zingine. Hata huduma za elimu, nyumba, maji, afya na umeme zimebinafsishwa.

Je, utekelezaji wa sera za ubepari umeathiri vipi tabaka la makabwela wa Tanzania? Washiriki wa kongamano la Nyerere walisema na kukubaliana kuwa ubinafsishaji wa uchumi kwa ujumla ni kinyume cha haki kwani unachukua mali inayomilikiwa na serikali kwa ajili ya wengi (umma) na kuwapa watu binafsi kwa kisingizio kimoja ama kingine. Marekebisho ya ubepari yamezidisha pengo kati ya matajiri na maskini, kupanda mbegu za uhasama wa kikabila  na kukiuka maadili ya kiutu yaliyozingatiwa na azimio la Arusha. Rushwa imekuwa dondandugu huku unyonyaji wa mtu kwa mtu ukiwa utamaduni wa kisasa. Wakati tabaka la wachache wanaotawala wakijilimbikizia utajiri mkubwa ajabu tabaka la Watanzania wengi linazidi kudidimia katika lindi la ufukara, shida na umkosefu wa kila hali. Washiriki kutoka Kenya, Malawi, Afrika Kusini na Uganda pia walisisitiza kwamba ubinafsishaji wa uchumi katika nchi zao pia umeleta manufaa kwa tabaka la wachache tu huku tabaka la wengi likizidi kusukumwa pembeni. Mwishowe kongamano liliamua kuwa ubepari umefeli Tanzania na pia Afrika Mashariki. Watanzania wengi hawana budi kupigania kurudi kwa Azimio la Arusha la siasa ya ujamaa na kujitegemea.

 

Mwandawiro Mghanga, Mwenyekiti wa Social Democratic Party of Kenya (SDP), Aprili 22, 2015

The future does not belong to imperialism. It belongs to the working class and t...
28 Apr 2026 12:35

Booker Omole is the General Secretary of the Communist Party Marxist Kenya, a Marxist Leninist and Maoist theoretician and organiser rooted in the struggles of the Kenyan working class and poor peasantry. He has played a leading role in rebuilding the communist movement in Kenya, advancing the line of the National Democratic Revolution, and spearheading ideological education, mass organisation, and anti imperialist mobilisation. Known for his uncompromising stance against neocolonial domination and revisionism, he has been at the forefront of political resistance, facing state repression while [ ... ]

Read more
The Anti Imperialist Struggle in West Asia and the World
28 Apr 2026 12:33

  Intervention by Booker Omole Sovintern English Language Forum, Moscow, April 2026   Comrades,   The question before us is not whether a wider war will emerge in what is referred to as the Middle East, a term of colonial origin which obscures the real geography of struggle.   The reality is that war is already unfolding in West Asia.   What we are witnessing is not a series of isolated conflicts, but the development of a unified and expanding system of imperialist war.   This system reflects the deepening crisis of imperialism as a global formation.   West Asia has become [ ... ]

Read more
The Reality of World War III and the Historic Task of Building the Anti Imperial...
28 Apr 2026 12:31

  Address by Booker Omole, the General Secretary of the Communist Party Marxist Kenya to the Sovintern Conference, Moscow, April 2026 Opening and Concrete Characterisation of the Present Conjuncture    Comrades,   We are not confronted with an abstract question of whether a new world war will emerge. We are confronted with the necessity of recognising the concrete form in which global war is already developing. The present international situation is defined by the transition from fragmented regional conflicts into an increasingly interconnected system of wars, driven by the structur [ ... ]

Read more
Giorgia Meloni’s Italy: The Criminalisation of Communism and the Return of Musso...
21 Apr 2026 08:19

21 April 2026   Comrade Paolo Babini is not a criminal. STATEMENT OF THE CENTRAL ORGANISING COMMITTEE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KENYA (CPMK) The Central Organising Committee of the Communist Party Marxist Kenya issues this unequivocal, militant and uncompromising statement in response to the ongoing political repression in Italy directed against Comrade Paolo Babini of the CARC Party.   We condemn in the strongest possible terms the raid carried out by the Italian police on the home of Comrade Paolo Babini in Florence, accompanied by the fabricated accusations of “terrorism” a [ ... ]

Read more