user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

On the 24th and 25th of May, 2014, Kenyans and fellow Africans from all walks of life will converge at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) Auditorium to commemorate the 51st anniversary of the Africa Liberation Day (ALD), with a symposium on the 24th of May, starting 10:30am-6:00pm, where among other topics in discussion will be the Decolonisation of Western Sahara, Resolving Wars on the continent, African Unity and the Role of Women in the Pan-Africanist struggles. The theme of this year's ALD is: "PanAfricanism-We Must Dare to Invent the Future" by Thomas Sankara.

There will be an open concert at the KICC courtyard starting at 1:00pm on the 25th of May, with performances from many progressive and conscious artists including Eric Wainaina, Afrizzo Band (Hellen Mtawali),Dr. Dan,Juliani, Sarabi Band, Maumau Vibrations (Ndungi Githuku), Grand Master Masese, Ukoo Flani, Vitalii (from Tanzania), Lam (from South Sudan), Sam Ondieki among many others.

Entrance for both events is free, open to all, and the Social Democratic Party is encouraging all its members and cadres to participate in this very important event on the Party’s calendar.

 

Below are Four Powerful Poems by Comrade Chairman Mwandawiro Mghanga,dedicated to this year’s ALD, that capture the spirit of African Liberation and Struggles.

Benedict Wachira – Secretary General

 

22nd May 2014

 

Tujenge Vyama vya Mapinduzi

Hebu viongozi niwasifu, wa kimapinduzi Afrika

Kwameh Nkuruma namsifu, ambaye Ghana alizalika

Na tena alikuwa marufu, kila taifa la Afrika

Kwameh ali jabali arifu, la ukombozi wa Afrika

Alikuwa akituarifu, haja ya umoja Afrika

Na alitenda mambo sufufu, ya ujamaa Afrika

Nkuruma alipoondoka, Ghana bepari wakachukua

 

Kuna Sekou Ture sikia, nchi ya Guinea ilitupatia

Wafaransa kumsikia, ah! wali wakijikojolea

Nkuruma alipomjua, komredi akajipatia

Na Ghana walipompindua, Conacry alikimbilia

Na pamoja wakapigania, Afriika kujikomboa

Ujamaa wakapambania, Guinea hata Afrika pia

Sekou alipotuondokea, Guinea ikatuharibikia

 

Madibo Keita nakwambia, Afrika alipigania

Na Mali alipozalikia, jina lake wanajivunia

Ni mzalendo alobobea, tena wa umma kupigania

Ukoloni aliuchukia, hata Kwameh alimtambua

Mali ya nyingi historia, pia Madibo aliichangia

Ujamaa aliwatakia, Wafrika kuushikilia

Ela alipoaga dunia, na Mali ikapotea njia

 

Naye Nyerere wa Tanzania, ni Mwafrika anosifika

Uhuru aliupigania, wa Tanganyika na Afrika

Ujamaa alizingatia, ni ukombozi wa Wafrika

Siasa ya kujitegemea, aliisema na kuandika

Mwalimu alitukariria, haja ya umoja Afrika

Na elimu ya kujikomboa, na Kiswahili kikajengeka

Nyerere alipoondoka, walochukua ni matapeli

 

Kuna Amilcar Cabral, alikuwa mwanamapinduzi

Wafrika walimkubali, kuwa shujaa wa ukombozi

Guinea Bissau ni yake asili, bali Afrika alienzi

Ujamaa mfumo halali, alifunza mwanamapinduzi

Alikuwa mwalimu kamili, wa nadharia ya mapinduzi

Hakuwa wa kuabudu mali, alipenda haki na mapenzi

Bali alipouawa mpenzi, na Guinea Bissau ikapotea

 

Agostino Neto sikia, ni mwanamapindizi Angola

Uhuru aliupigania, huku ujamaa akilola

Mabeberu walimchukia, wakamfanyia kila hila

Bali Neto aliendelea, hakukatishwa tama na dhila

Mashairi alituwachia, ya uhuru na haki kulola

Umoja Afrika kukua, Neto alipinga ukabila

Lakini Neto alipolala, na Angola kombo ilienda

 

Samora Macheli nampenda, ni Msumbiji alizaliwa

Na Afrika aliipenda, na pia siasa za usawa

Ndiyo mana jeshi wakaunda, la Msumbiji kuikombowa

Ndipo vita walipovishinda, ujamaa ukanza kukuwa

Vyema mambo yakaanza kwenda, mfumo wa utu wa usawa

Kusini Afrika akenda, kuchangia nchi kuzikombowa

Ela Samora alipowawa, Msumbiji huna mwelekeo

 

Na hayo hayakuanza leo, tukumbuke Kenya mashujaa

Mau Mau hadi hivi leo, twakumbuka waliwasha taa

Afrika kwenda mbiombio, kwa ukombozi wa kisilaa

Siasa za kimaendeleo, za utaifa uje kukaa

Hii hali iliyoko leo, wengi maisha ya kalabaa

Mau Mau ilipinga hayo, wao ni mfumo wa kufaa

Bali bado kale wanakaa, na kupambana wamesimama

 

Mandela ni shujaa mwadhama, mtu mwema sana duniani

Ni kiongozi mwenye hekima, ali marufu ulimwenguni

Tangu ujana hadi uzima, kwa uhuru au kifungoni

Haki Mandela alitazama, na usawa kweli na amani

Alikuwa mfano mwema, kote na Afrika Kusini

Alitakia wote salama, akipigania maskini

Tulipomueka kaburini, mafisi wa ANC tayari

 

Na pia huko nchi ya Misri, kuli na kiongozi hodari

Tena alikuwa mashuhuri, kupinga ubeberu kwa ari

Afrika wende ubepari, uhuru wapate amfari

Mashariki ya Kati uhuri, Abdi Naser alikariri

Mfumo ujamaa Misri, mwanapinduzi alihubiri

Kwa Naser Afrika nzuri, ni muungano kuwa tayari

Ela alipokufa si siri, imeenda kikombo Misri

 

Na huko nchi ya Algeria, Ben Bela ali ni hodari

Nchi yake aliipambania, na wazalendo majemedari

Mashujaa wa Algeria, waliupigania uhuri

Wafaransa wakakimbia, wakakimeza chao kiburi

Afrika alifikiria, huku akipinga ubepari

Ukombozi alisaidia, kwa silaha na kwa kila hari

Bali alipowekwa kwa kaburi, Algeria ni ubepari

 

Afrika ni kweli si siri, unazoroteka uongozi

Watawalao ni mabepari, watu wasojali mapinduzi

Watu walafi wenye kiburi, wasiyo na utu na mapenzi

Wanaozalisha ufakiri, kwa sera katili za kishenzi

Ndiyo, kwa heri ama kwa shari, lazima tulete uongozi

Wa kupambana na ubepari, historia nzuri kuenzi

Kuwa mapinduzi endelezi, tujenge vyama vya mapinduzi

 

Mwandawiro Mghanga, Kahawa Sukari, Februari 5 2014

  

Maliasili za Afrika!

Afrika rasilimali, ni bara limebarikiwa

Madini ni kila pahali, hata kawi tumejaliwa

Na misitu pia ni mali, kwa maumbile tumepewa

Tuna bahari kwa maili, maliasili zimejawa

Utajiri tumejaliwa, na Afrika ni fukara!

 

Wafrika ni mafukara, na tunazo maliasili

Kutoka pwani hadi bara, tilatila maliasili

Tunapigwa kama mpira, na ni zetu maliasili

Tunaporwa maisha bora, tukiporwa maliasili

Zimejaa maliasili, bali ukiwa unakua!

 

Ukiwa umetuzidia, na tunazo maliasili

Ulaya wanafaidia, kutokana na zetu mali

HataUchinana India, wanazijasiriamali

Amerika washikilia, kutupora maliasili

Hatuoni cha afadhali, Wafrika ni masikini!

 

Tunabakishwa masikini, na tuna mzo utajiri

Mali za chini ardhini, tilatila za kila mbari

Zinaenda ughaibuni, kuzalishia utajiri

Sisi twatoa mchangani, kuwapatia mabepari

Tunabaki na ufakiri, Afrika tunaumia!

 

Afrika tunaumia, tunabaki ’kusaidiwa’

Wageni wanatutumia, maliasili twaibiwa

Na huku wakituibia, viongozi wanatumiwa

Mabepari wafurahia, na umma unasalitiwa

Maliasilitwaibiwa, usalitiwaviongozi!

 

Usaliti wa viongozi, wanatuuza Wafrika

Ulafi wao viongozi, wa mabeberu vibaraka

Walimi na wafanyikazi, maisha yamejaa shaka

Maliasili ni machozi, badala ya kuwa baraka

Uongozi wa vibaraka, maendeleo unapinga

 

Maendeleo unapinga, wa vibaraka uongozi

Tunafanywa watu wajinga, na wa ughaibuni wezi

Mana viongozi wajinga, wanatuuza waziwazi

Uhuru wetu wakipinga, tukililia ukombozi

Imekuwa mali ya wezi, maliasili Afrika!

 

Maliasili Afrika, Wafrika wazimiliki!

Chumi zipate kufufuka, za kuokoa halaiki

Tuwaondoe vibaraka, tuwe na mfumo wa haki

Ikiwa si kwa Wafrika, bora mchangani zibaki

Badala fukara kubaki, tukiporwa rasilimali!

 

Lazima tuseme ukweli, tunahitaji mapinduzi

Tutumie zetu akili, tusifaidi mabazazi

Watupore rasilimali, na tukiwa wafanyikazi

Watunyonye kwa zetu mali, kwa usaliti uongozi

Lazima yawe mapinduzi, Afrika inahitaji!

 

Mwandawiro Mghanga, Kahawa Sukari, Machi 18 2014

 

Swala la Uongozi Afrika

Ni swala nyeti uongozi, Kenya yetu na Afrika

Ili tupate ukombozi, uhuru uweze kufika

Maongozi na uongozi, ni lazima kubadilika

Mana ni jambo lilo wazi, bara letu lafilisika

Kwa kuwakosa viongozi, ambao wanahitajika

Twaongozwa na mabazazi, wasaliti na vibaraka

Tunahitaji mapinduzi, viongozi kujipatia

 

Viongozi kujipatia, ni shabaha ya mapinduzi

Umma wanaofikiria, binadamu wenye mapenzi

Haki wanaozingatia, wa kuondoa ubaguzi

Wa ukweli kushikilia, wajibikaji na uwazi

Ambao watu wakilia, na waohutoa machozi

Na siwahalifu sikia, kama waleo majambazi

Lazima tutafute njia, tupate viongozi wema

 

Tupate viongozi wema, ilitupate endelea

Sababu leo tumekwama, kwahakika tumepotea

Kwa maongozi ya dhuluma, ufisadi ulokolea

Viongozi bila heshima, kazi yao ni kunyakua

Ni mafisi ninaosema, wako kujilimbikizia

Hata taifa likizama, hawajali nakuambia

Wanauza wao mama, hawa ni viongozi gani?

 

Waabudu pesa mashetani, ndiyo viongozi wa leo

Ni watu mfano majini, wanyama viongozi hao

Wametufanya masikini, tuyakatae mambo yao

Ya ubepari ukoloni, twangushe na mfumo wao

Tuwang’oe uongozini, ndiyo kuwe maendeleo

Tujiulize ni kwa nini, bado tunachagua wao!

Tufikirie kwa makini, hujaje wawe viongozi?

 

Tunahitaji mapinduzi, sisi wenyewe sikia

Wenyewe twachagua wezi, nakisha huku tunalia

Au tunafanya upuzi, chaguzi kutozingatia

Sharti tuifanye kazi, ni sisi tutajikomboa

Ikiwa njia niuchaguzi, tupige kwa kufikiria

Kama njia ni mapinduzi, tukubali kujitolea

Mana swala la uongozi, ni swala la ukombozi

 

Mwandawiro Mghanga, Dream Hotel Ngara, Alhamisi  Mei 15 2014

 

 Ukombozi ni Mapambano

Kila siku tunalilia, kupata mfumo mzuri

Wa haki kwa kila raia, salama na kila la heri

Utu wa mtu kujalia, na kuondoka ufakiri

Hata ukabila pia, ukagura na zake shari

Usawa wa kijinsia, na kujali kila umri

Ni ndoto tunajiotea, mambo mema kuyafikiri

Bali bila kupambania, ndoto zetu hazijiri

 

Kwa hakika hayatajiri, pasipo kupambania

Hadi tuwe na uhodari, kwa uwoga kuuondoa

Bila kujiweka tayari, tutakayo kupigiania

Tutabaki kwa ufakiri, katika ndoto kuselea

Kila siku tunafikiri, na ufisadi wendelea

Tupambanie nakariri, ndio yawe tunolilia

Ili mambo yawe tayari, kujizatiti fikiria

 

Tumejaza Kenya tabia, ya kukaa na kufikiri

Sera nzuri kujipangia, na kujichorea mazuri

Kisha pia kuombea, Mwenyezi tukitafakari

Misikitini kuswalia, na makanisa forofori

Kwa maombi kutujalia, bila sisi kutia ari

Ni bure hayatakua, bila juhudi hayatajiri

Haki ni kupigania, na hili si jambo la siri

 

Hapatii bure bepari, haki kwao wafanyikazi

Hana huruma mwaajiri, mabepari ni mabazazi

Kujiongeza utajiri, kwa kunyonya wafanyikazi

Hajaye ukue mtaji, mengine kwake ni upuzi

Alazimishwe bepari, na vita vya wafanyikazi

Kwa umoja wakiwa hodari, haki zao watamaizi

Ni sharti tuwe tayari, kupigania ukombozi

 

Na mapambano ni kazi, ni juhudi za kujitolea

Chama kuoganaizi, na mikakati kupangia

Malengo bora kumaizi, na uwoga kuuondoa

Tukijizatiti kwa kazi, hatimaye tutatoboa

Ni kama vya kimapinduzi, vita ninavyosimulia

Kuiondoa simanzi, ya nyanyaso kuvumilia

Ni kuwa tayari kwa kazi, jambo hili nalirudia

 

Tukumbuke historia, ili ukweli kuujuwa

Mwanzo wakituvamia, vita vikubwa vilikuwa

Wakoloni waliwajua, wazalendo waliyokuwa

Na ili uhuru kungia, Wakenya kujikombowa

Ilibidi kupigania, kwa mapambano kunyakuwa

Na hata demokrasia, ilibidi kupambaniwa

Mana bila kujitolea, tutagandamizwa milele

 

Hali itawa vilevile, tukingojea wa bwerere

Tulalamike na tulile, bila kupigania ni bure

Watatukalia milele, tusipotoka na mishare

Tukitaraji kwenda kule, kufika kwa jamii shware

Ni lazima huku na kule, chama kijae forifore

Haki haziji kwa fadhile, au huruma za bepare

Ni tangu zamani za kale, haki haziji burebure

Kwa beti hizi nakaririle, uhuru ni kuwa tayare

 

 Mwandawiro Mghanga, Kahawa Sukari, Januari 24 2014

  The Rural Woman: Not to Be Celebrated—But Liberated
24 Nov 2025 06:00

                                                                  peech on the Peasant Women Day, 15th October, 2025. Written by Leon Munala Secretary of The Peasants and Peasant Organization Delivered by Comrade Karimi Wa Kagendo National Organising Secretary, Revolutionary Youth League Comrades, sisters, and fellow workers! Today, the representatives of global capital in their glass palace tells us to celebrate. The United Nations, that grand committee for managing the common affairs of the global bourgeoisie, has  [ ... ]

Read more
FROM THE COMMUNE TO THE PEOPLE’S POWER: ANTI-IMPERIALIST STRUGGLE AND THE PATH O...
12 Nov 2025 08:41

    Booker Omole General Secretary, Communist Party Marxist Kenya (CPMK) October 17th, 2025 Caracas, Venezuela   omuna o Nada: The Question of Power in the Age of Imperialist War Comrades, the slogan “Comuna o Nada” — the commune or nothing — is not merely a Venezuelan proclamation; it is a universal cry of the proletariat in our epoch of crisis. It affirms that without transforming the relations of production, without uprooting imperialist domination, and without transferring power from the exploiting classes to the working people, there can be no socialism.   Today, [ ... ]

Read more
OFFICIAL STATEMENT ON THE FASCIST OFFENSIVE OF IMPERIALISM IN TANZANIA UNDER PR...
05 Nov 2025 14:01

November 2, 2025   The Communist Party Marxist Kenya stands with the people of Tanzania in this moment of heightened danger. The ruling class across East Africa is tightening the chains of monopoly finance capital. The mask of liberal democracy is falling. Behind it stands naked reaction. Behind it stands fascism in African colours.   President Samia Suluhu Hassan has presided over political developments marked by aggressive interference from foreign capital. We are witnessing new assaults by the corporations and financial institutions headquartered in the old imperial centres. They want [ ... ]

Read more
STATEMENT ON THE PASSING OF COMRADE KIM YONG NAM COMMUNIST PARTY MARXIST KENY...
05 Nov 2025 13:51

    November 5, 2025   The Communist Party Marxist Kenya conveys its deepest condolences to the Workers Party of Korea, the Government of the Democratic People’s Republic of Korea, and the heroic Korean people on the passing of Comrade Kim Yong Nam, former Chairman of the Standing Committee of the Supreme People’s Assembly.   Comrade Kim Yong Nam was not merely a statesman. He was a defender of sovereignty. He was a guardian of independence. He was a steadfast revolutionary in the global front against imperialism.   Throughout his service to the Party and the State, the Dem [ ... ]

Read more